MATANGAZO YA WIKI 27 JULAI — 02 AGOSTI 2026
Attachment Available
27-july-02-aug-2026_20260725_201046.pdf
VIONGOZI WA ZAMU
27 JULAI — 02 AGOSTI 2026
MCHUNGAJI
MCH. JOSEPH ENOS 0652 889 852
MZEE WA KANISA: MRS. NATUJWA WINZAH
WAZEE NA MAKATIBU WAO WATAKAOKU WA ZAMU, KUABUDU IBADA ZOTE MBILI SIKU YA JUMAPILI IJAYO TAREHE 02/8/2026:
MR. ALFA BYAMUNGU
MRS. THERESIA MWABUSILA
DR.CHRISTIAN MEIKARE
MASHEMASI WA ZAMU:
MRS. ASNATH KAMANGA
MR. ATHANAS MPONZI
MRS. ATUGANILE ANDREW
MR. BASILI MKINI
MATANGAZO
Wazee wote wenye mitaa mnahimziwa kutembelea vituo vyenu vya HBCF ili kujua maendeleo ya vituo hivyo na kuviimarisha, wakisaidiana na makatibu pamoja na mashemasi.
Mchungaji Kiongozi anakumbusha tena kuwa vijana ambao wako kwenye mahusiano ya uchumba wasikae zaidi ya miezi mitatu bila kuonana na Mch. Dickson Mkoka pia wajitambulishe kwenye kamati ya kushauri chumba na kuhudhuria kwenye vikao vya chumba.
MABADILIKO YA RATIBA YA CMF
Ibada ya CMF hapa kanisani kwa sasa itaanza kuanzia saa 12 jioni hadi saa 1 usiku ni maombi, saa 1 usiku hadi saa 2 usiku ni neno la Mungu. Wanaume wote mnahimizwa kushiriki.
MICHANGO YA FEDHA ZA UJENZI
Kwa neema ya Mungu ujenzi wa kanisa letu unaendelea, hivyo unatiwa moyo wewe uliye ahidi mchango wa ujenzi kwa awamu hii ya sita B kutoa au kupunguza ahadi yako ili kazi ya ujenzi iendele. Kumjengea Mungu nyumba ya ibada ni baraka kwako na kwa vizazi vyako.
Unaweza kutuma mchango wako kwenda namba:
015 0020374000 CRDB BANK.
Jina: KINONDONI REVIVAL CHURCH
PAA LA KANISA, MUUJIZA WANGU
ZAMU ZA MAOMBI YA WATENDAJI
Watendaji wote wa kundi la NAZARETH mtakuwa zamu ya mfungo na maombi siku ya Jumamosi ijayo ya tarehe 01/08/2026. Watendaji wote waliopo maeneo ya Mr. Paul Tarimo,Mr. Roderick Lutembeka, na Mrs. T. Mwabusila.
MKUTANO MKUBWA WA INJILI
Kutakuwa na Mkutano mkubwa wa Injili katika viwanja vya Mwananyamala kwa Kopa kuanzia Tarehe 30 Augusti hadi 06 Septemba 2026 Washirika wote tunahimizwa kuuombea Mkutano na pia tujipange kushiriki kikamilifu kwa siku zote nane (8)
TANGAZO LA NDOA
Kwa mara ya kwanza tunatangaza harusi kati ya kaka Anyitike Enock Mwangungulu na dada Fortunata Gideon Patrick wote ni washirika wa TAG Kinondoni Harusi itafanyika siku ya Jumapili tarehe 26/08/2026 hapa kanisani TAG Kinondoni