MATANGAZO YA WIKI  03 -  09 AGOSTI 2026
arrow_back All Announcements
weekly push_pin Pinned

MATANGAZO YA WIKI 03 - 09 AGOSTI 2026

calendar_today August 01, 2026 person Super Admin
picture_as_pdf

Attachment Available

03-09-aug-2026_20260801_190221.pdf

download Download PDF

VIONGOZI WA ZAMU AUGUST 2026

MCHUNGAJI

MCH. WITNESS SWAI 0629 534 530

MZEE WA KANISA

MR. MATHIAS MSANGI

WAZEE NA MAKATIBU WAO WATAKAOKU WA ZAMU, KUABUDU IBADA ZOTE MBILI SIKU YA JUMAPILI IJAYO TAREHE 09/8/2026

MCH. YOTHAM MACKENZIE

MCH. DICKSON MKOKA

MR. JOSEPH MAMUYA

MASHEMASI WA ZAMU

MRS. BEATRICE MLIMBILA

MR. CASTORY KUTIKA

MR. CLEMENT ZONGELA

MR. CHRISTIAN CHARLES

MATANGAZO

  1. Wazee wote wenye mitaa mnahimziwa kutembelea vituo vyenu vya HBCF ili kujua maendeleo ya vituo hivyo na kuviimarisha, wakisaidiana na makatibu pamoja na mashemasi.

  2. Mchungaji Kiongozi anakumbusha tena kuwa vijana ambao wako kwenye mahusiano ya uchumba wasikae zaidi ya miezi mitatu bila kuonana na Mch. Dickson Mkoka pia wajitambulishe kwenye kamati ya kushauri chumba na kuhudhuria kwenye vikao vya chumba.

  3. Tarehe 07/08/2026 yaani Ijumaa ijayo, Kutakuwa na mkesha wa vijana wote katika Section Yetu ya Kijitonyama, ambao utafanyika hapa TAG Kinondoni. Hivyo: vijana wote mnahimizwa kushiriki mkesha huo.

MICHANGO YA FEDHA ZA UJENZI

1.Kwa neema ya Mungu ujenzi wa kanisa letu unaendelea, hivyo unatiwa moyo wewe uliye ahidi mchango wa ujenzi kwa awamu hii ya sita B kutoa au kupunguza ahadi yako ili kazi ya ujenzi iendele. Kumjengea Mungu nyumba ya ibada ni baraka kwako na kwa vizazi vyako.

2.Unaweza kutuma mchango wako kwenda namba:

015 0020374000 CRDB BANK. Jina: KINONDONI REVIVAL CHURCH

PAA LA KANISA, MUUJIZA WANGU

ZAMU ZA MAOMBI YA WATENDAJI

Watendaji wote wa kundi la YERIKO mtakuwa zamu ya mfungo na maombi siku ya Jumamosi ijayo ya tarehe 08/08/2026. Watendaji wote waliopo maeneo ya Mch Bryson Kitoi, MrsNatujwa Winzah, Mr. Mathias Msangi na Dr. Christian Mollel.

MKUTANO MKUBWA WA INJILI

Kutakuwa na Mkutano mkubwa wa Injili katika viwanja vya Mwananyamala kwa Kopa kuanzia Tarehe 30 Augusti hadi 06 Septemba 2026 Washirika wote tunahimizwa kuuombea Mkutano na pia tujipange kushiriki kikamilifu kwa siku zote nane (8)

TANGAZO LA NDOA

Kwa mara ya pili tunatangaza harusi kati ya kaka Anyitike Enock Mwangungulu na dada Fortunata Gideon Patrick wote ni washirika wa TAG Kinondoni Harusi itafanyika siku ya Jumapili tarehe 26/08/2026 hapa kanisani TAG Kinondoni.

MABADILIKO YA RATIBA YA CMF

Ibada ya CMF hapa kanisani kwa sasa itaanza kuanzia saa 12 jioni hadi saa 1 usiku ni maombi, saa 1 usiku hadi saa 2 usiku ni neno la Mungu. Wanaume wote mnahimizwa kushiriki.